Chemichemi Za Uzima




MSTARI WA LEO

Muhubiri 7:14
Siku ya kufanikiwa ufurahi,
Na siku ya mabaya ufikiri.
Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili,
ili mwanadamu asipate kulijua neno lolote litakalofuata baada yake.



Kwa maombi na maombezi au msaada wowote wa kiroho wasiliana nasi kwa;
Simu Namba: +255 756 066 011; +255 688 891 469; +255 752 184 464; au
Barua pepe: chemichemizauzima11@gmail.com; tulbundala@gmail.com

Bofya hapa kutembelea ukurasa wetu facebook na Ulike

Bofya hapa kututembelea youtube na uangalie video zetu za mafundisho ya Biblia na Ibada zetu

Wednesday, 22 January 2014

Aponywa Jipu Papo kwa Papo katika kitovu chake baada ya kufanyiwa maombi kwa njia ya Simu ya mkononi

Mama Nteze akiwa anashuhudia katika ibada mojawapo ya Jumapili akimshukuru Mungu kwa uponyaji alioupata mara tu baada ya kuombewa kwa njia ya simu.

Mama huyu aliyekuwa na jipu kubwa katika kitovu chake ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda wa miezi saba aliponywa papo kwa papo kwa maombi yaliyofanyika kupitia simu yake ya mkononi. Mama huyu, alikuwa anasikiliza kipindi cha redio kinachokwenda kwa jina la Chemichemi za Uzima, kinachoongozwa na Mchungaji Emmanuel N. Manweli na mke wake Mchungaji Chatherine Manwele wa Kanisa la Chemichemi za Uzima, Calvary Assemblies of God Area A Dodoma. Akiwa anaendelea kusikiliza mafundisho na mahubiri, muda wa maombi uliwadia, ndipo alipoamua kuchukua simu yake na kupiga. Mama huyu alieleza shida yake, kuwa anasumbuliwa na jibu bichi katika kitovu chake kwa muda wa miezi saba (7); Mchungaji alimuambia baada ya kusikiliza shida yake kwamba aweke mkono wake mahali penye jipu na kuuondoa mara tatu; alipoutoa mkono wake mara tatu, alifunua tumbo lake, kumbe! jipu lilikuwa limekauka pale pale.

Haya ndio matendo ya Mungu ya ajabu. Mpendwa, siku chache zijazo tutaanza kukuletea video za shuhuda hizi, ili uone jinsi Mungu aponyavyo na kufungua watu wake.

No comments:

Post a Comment


Tunakushukuru kuwa sehemu yetu!                                                                                                Mungu Akubariki Sana

Kwa maombi na maombezi au msaada wowote wa kiroho wasiliana nasi kwa;
Simu Namba: +255 756 066 011; +255 688 891 469; +255 752 184 464; au
Barua pepe: chemichemizauzima11@gmail.com; tulbundala@gmail.com